TAFAKURI

UJUMBE WA LEO
Soma mpaka mwisho utajifunza kitu
Kulikua na mtu mmoja mpasua mawe

Mtu huyu aliichukia sana Kazi yake na kuona ni ngumu na nikama anaonewa kwa Kazi hiyo japo ni jukumu lake na anatakiwa aifanaye ili apate kuishi 
Siku moja akiwa anapasua mawe aliona mtu akiwa amebebwa, akiwa amekalia kiti cha thamani na watu wakimwimbia kwa shangwe sana. Akaenda kutambua mtu yule ni mfalme 

Bwana huyu alitamani sana na kujisemea Mungu akimfanya mfalme bhasi yeye maisha yake yatakua mazuri na ataridhika kabsa.

Kimuujiza ghafla akawa mfalme na watu wakawa wanamwimbia na kumchezea sana, bwana yule alifurahi sana na aliwaagiza wtumishi wake kumtembeza kila atakapo na kila saa.

Lakini akiwa amebebwa na huku anaimbiwa sana alichomwa sana na jua maana ilikua nikipindi chakiangazi, lile jua nilikua Kali sana na lilimkera, mtu yule akasema

"kumbe hata ufalme sio kitu!!!? Yaani ningekua tyu jua bhasi Mimi ndo ningetawala ningeridhika kabsa.

Ghafla bwana yule akawa jua. Kwa kweli alifurahi sana aliwaka kwa kiwango kikubwa, alichoma mazao sana na kuyaharibu ali maisha dunia na sasa kila kitu kikawa kimekauka miti inaanguka, wanyama wanakufa kwa kweli alikua anasababisha jangwa.

Lakini wakati anachoma sana kila kitu kilipata shida na alifurahi, lakini akaona jiwe mahali hilo jiwe kwanzia ameanza Kazi yake jiwe lile halikusogea wala kupata shida yeyote akaamua kuliwakia kisawasawa na kulichoma sana lakini jiwe lile halikutikisika ni kama unafanya Kazi bure.

Wakati amechoka kabsa akajisemea "haaa! Inamaana hata jua sio kila kitu bhasi jiwe ndo kila kitu. Ningekua jiwe mimi bhasi ningeridhika."

Ghafla akawa jiwe, bhasi kwakweli alikaa kwa Amani jua liwake, mvua inyeshe, mtu alikalie hasikii kitu kabisa.

Akiwa anafikiria kua imetoshea ghafla alitokea mpasua mawe na nyundo yake, alipiga Mara ya kwanza na Mara ya pili jiwe likapasuka. 

Bwana yule alighadhabika sana na kujisemea "bhasi jiwe sio kila kitu, huyu mpasua mawe ndio kila kitu, nataman ningekua mpasua mawe."
Ghafla akawa mpasua mawe ambayo ndio Kazi yake ya mwanzo......

FUNZO 

kila wakati tumekua tukitamani kuwa flani, au kuwa na maisha ya namna flani na katika kugombea hali hiyo tumejikuta tukimtenda Mungu dhambi za aina nyingi, tumesahau ipi njia sahihi ya mafanikio.

Njia ya pekee ya kufanikiwa au kuishi maisha flani ni yesu pekee, ni kumwamini Mungu wa mbinguni, mungu wa Ibrahim, isaka na Yakobo yeye pekee ndiye anaye tosha. Badilisha njia zako na Maputo yako mrudie bwana na mwombe yeye atajibu
Mimi


naamini na ninaomba Mungu awe dereva wa maisha yangu. 

Kama nawe unaamini andika AMINA 
Na ikiwezekana share kwa wengine wajifunze. Utabarikiwa kuliko unavyofikiri.
Mungu wa mbinguni akubariki.



For English click Here

Comments

Popular posts from this blog